Msakamaboga
Msakamaboga

@msakamaboga

6 Tweets 93 reads Jul 01, 2023
DM ZIMEKUWA NYINGI.
PITIA UZI
#RT
FREE PROJECT (PHARMACY)
(MTAJI 10M)
#MAHITAJI
1) MTAJI (10M)
2) ENEO (JENGO/NYUMBA)
3) WAHUDUMU
a) PHARMACIST
b) pharmaceutical Technician
4) KIBALI CHA KUENDESHA BIASHARA (PC NA TRA)
5) NAMNA YA KUENDESHA BIASHARA
6) BIDHAA (DAWA)
1) MTAJI ( 10)
Inahitajika Mtaji wa million Kumi kufanya uwekezaji wa Pharmacy ya Reja Reja tu, Nenda na Uzi uone mchanganuo wake.
2) ENEO/JENGO/NYUMBA
jengo la kuanzisha biasha ya Pharmacy linatakiwa liwe lenye uwezo wa kuweka store na sehemu ya kuuzia Dawa, na linakaguliwa.
Baada ya kupata jengo lenye vyumba viwili vikubwa litafanyiwa ukaguzi kama litakidhi vigezo watakupa utaratibu au kibali cha kuanza ukarabati wa jengo lako.
KODI KWA MIEZI 6 INAWEZA KUWA 600K OR 750000 (MAELEWANO) KAMA SIO MJINI SANA. lakini pia kwenye ukaguzi wanazingatia umbali
Wa Pharmacy Moja na nyingine (zingatia) japo mjini sio sana
MAHITAJI YA JENGO
1) KABATI
hizi zipo za aina mbili
A) vioo
B)Mbao
Kwa sababu mtaji wetu ni mdogo naona tutumie Mbao kwenye ku design ambazo gharama yake sio kubwa kama vioo angalia mifano
Ingawa ukarabati wa sehemu ya store sio kama wa kuuzia Dawa.
Kikubwa uweke (SHELVES NA PELLETS)
2)FENI AU AIC
3) DESIGN YA JUU , TAA, SYSTEM ZA UMEME, MEZA, N.K VITI VYA WA TUMISHI NA KIMOJA CHA WAGONJWA (wateja), angalia mifano
pamoja na kupa rangi nyeupe kwenye Kuta) na VIGAE
Lakini kama pharmacy inatakiwa iwe na DDA BOX kabati la kutunzia Dawa maalumu kama Dawa za kifafa, ganzi, maumivu makali, kansa n.k hakina gharama kubwa kwa sababu ni kidogo sana, unaweza kuhitaji fridge japo sio lazima kama huuzi Dawa zenye huitaji wa hivyo vifaa.
GHARAMA 3.5M
WAHUDUMU NA MISHAHARA YAO
ili uweze kupewa kibali cha kuendesha biashara ya Pharmacy lazima uwe na watu hawa
1) PHARMACIST mshahara per month
Inategemea na makubaliano yenu
2) Pharmaceutical Technician mshahara wake per month inategemea na makubaliano yenu

Loading suggestions...